SIKU YA – 10:
KRISTO AKIAKISIWA KWA MAJIRANI:
"Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi." Matendo 1:8
Anzeni kipindi cha maombi kwa kumsifu Mungu kwamba ni mwema, mwenye fadhili na mpole.
Mtukuze Mungu kwamba amechagua kukutumia wewe kuzifikia roho ambazo zina kiu ya maji ya uzima.
Kuungama na Kudai Ushindi dhidi ya dhambi.
Muombe Mungu akuonyeshe dhambi unazohitaji kuziungama kwa wazi na zile unazohitaji kuziungama kwa siri.
Dai ushindi Wake dhidi ya dhambi hizo.
Omba kwa ajili ya msamaha kwa nyakati ambazo uliona haya kushiriki imani yako kwa wengine.
Muombe Mungu akupatie ujasiri na upendo kupitia Kristo kukaa ndani yako.
Mshukuru Mungu kwamba anakusamehe kulingana na 1Yohana 1:9
Sala na Maombezi. Muombe Mungu akupatie mzigo wa kuongoa roho na upendo kwa watoto Wake waliopotea.
Muombe Mungu aweke katika mioyo ya majirani zako njaa na kiu Yake.
Muombe Bwana akujaze na Roho wake Mtakatifu na akufundishe jinsi ya kuwafikia majirani kupitia matendo yako ya upendo, kwa kuhudumia mahitaji yao, kwa wao kukuamini, na kwa kuwaalika kumfuata Yesu.
Omba ili uweze kushiriki uzoefu wa furaha ya kumtangaza Yesu.
Omba kwa ajili ya tabia yenye kupendeza, tabia kama ya Kristo ambayo itawavuta watu kwa Yesu.
Omba ili Mungu akufundishe jinsi ya kuwaelekeza watu kwa Yesu na si kwako mwenyewe.
Omba kwa ajili ya matumizi zaidi ya vitabu vya Kikristo kwa washiriki wote na kwa mkazo zaidi katika uinjilisti wa vitabu, kupitia kwa nakala zilizochapishwa na ambazo ziko katika namna ya kielektroniki.
Omba kwa ajili ya mkazo mpya juu ya umuhimu mkubwa wa kuhudhuria Shule ya Sabato, ambayo inalenga katika ushirika, utume, kujifunza Biblia na huduma nje ya kanisa.
Omba kwa ajili ya mkazo zaidi kwa vikundi vidogo vya kutoa huduma nje ya kanisa, ili washiriki wote waweze kujihusisha katika ushuhudiaji binafsi na kutangaza ukweli mkuu wa Mungu katika siku hizi za mwisho.
Omba ili viongozi wa kanisa (mchungaji wako wa Mtaa, wachungaji wa konferensi, unioni, divisheni na Makao Makuu ya Kanisa waweze kuwa mashahidi wazuri kwa majirani zao.
Utume katika miji Mikuu –
omba kwa ajili ya divisheni ya Inter-Europian na miji waliyoichagua kuifanyia kazi: Geneva, Prague, Vienna. Inua katika maombi pia Unioni za Middle East na North Africa na miji 43 wanayopanga kuifikia katika miaka mine hadi mitano ijayo.
Ombea washiriki wanaofanyia kazi miji hii.
Muombe Mungu kwa ujasiri wa kumshuhudia Yeye katika mazingira yo yote yale.
Omba kwa ajili ya kukua kwa lengo katika huduma ya vyombo vya habari vya kanisa, vikiongoza katika uinjilisti mkubwa wa ushuhudiaji kote duniani.
Omba kwa ajili ya watu saba au zaidi katika orodha yako ili kwamba waone hitaji lao na kufungua mioyo yao kwa Roho Mtakatifu.
Omba kwa ajili ya mahitaji binafsi uliyo nayo.
Shukrani
Mshukuru Mungu kwamba anatenda kazi katika maisha ya watu wa familia yako, marafiki na majirani.
Mshukuru Mungu kwamba anao watu katika kila mji ambao wanatazama mbinguni kwa shauku kuu!
Mshukuru Mungu kwamba anafanya kazi katika mioyo ya wale ambao umekuwa ukiwaombea.
Mapendekezo ya Nyimbo:
Tawala ndani yangu no.147, Taa yangu ndogo nitaiangaza, Walio kifoni no.56, Kuwatafuta wasioweza no.100
"Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi. Matendo 1:8
Watoto wa Mungu wanaitwa wawakilishi wa Kristo, wakionyesha wema na rehema za Bwana. Kama Yesu alivyotufunulia tabia ya kweli ya Baba Yake, nasi tunapaswa kumfunua Kristo kwa ulimwengu ambao haujui upendo Wake wenye upole na huruma. “Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni,” alisema Yesu, “nami vivyo hivyo naliwatuma hao ulimwenguni.” “Mimi ndani yao, nawe ndani yangu;…..ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma.” Yohana17:18,23. Mtume Paulo anawaambia wanafunzi wa Yesu, “Mnadhihirishwa kwamba mmekuwa barua ya Kristo,” inajulikana na kusomwa na watu wote.” 2Wakorintho3: 3, 2. Katika kila mtoto wa Mungu, Yesu anatuma barua kwa ulimwengu. Kama wewe ni mfuasi wa Kristo, anatuma kupitia kwako barua kwa familia, kijijini, barabarani, mahali unapoishi. Yesu, ndani yako, anatamani kuongea na mioyo ya wale ambao hawamtambui. Huenda labla hawasomi Biblia, au hawaisikii sauti inayoongea nao katika kurasa za Biblia; hawaoni upendo wa Mungu kupitia kwa kazi Zake, lakini wewe ni mwakilishi wa kweli wa Yesu, yaweza kuwa kupitia wewe, wataongozwa kuelewa jambo fulani la wema Wake na kuvutwa kumpenda na kumtumikia Mungu.
Tembelea majirani zako na onyesha kujali wokovu wa roho zao. Amsha kila uwezo wa kiroho katika utendaji. Waambie wale unaowatembelea kwamba mwisho wa mambo yote u karibu. Bwana, Yesu Kristo atafungua milango ya mioyo yao na atafanya katika akili zao mvuto utakaodumu. Hata wakati wanapojishughulisha na kazi zao za kila siku, watu wa Mungu wanaweza kuongoza wengine kwa Kristo. Na wakati wanapofanya hili, watakuwa na uhakika wenye thamani kwamba Mwokozi yupo karibu nao. Hawahitaji kufikiri kwamba wameachwa kutegemea juhudi zao dhaifu. Kristo atawapatia maneno ya kuongea ambayo yataburudisha na kutia moyo na kutia nguvu walio maskini, na roho zinazotaabika katika giza. Imani yao wenyewe itatiwa nguvu wanapotambua kwamba ahadi ya Mwokozi inatimizwa. Wao sio tu mbaraka kwa wengine, bali kazi wanayoifanya huleta mbaraka kwao wenyewe.
Mvuto wako hufikia nafsi; unagusa waya ambao si waya wa kawaida bali waya unaotetema kwenda kwa Mungu…. Ni wajibu wako kuwa Mkristo wa viwango vya juu vya neno, “kama Kristo”. Ni kupitia kwa mistari isiyoonekana inayokuvuta kwa akili za watu wengine ambao unakutanishwa pamoja nao, kwamba kama unadumu katika muunganiko na Mungu, utaacha mivuto ambayo itakufanya kuwa “harufu ya uzima iletayo uzima” Bali, kama wewe ni mbinafsi, kama unajiinua mwenyewe, kama akili yako ni ya kidunia, haijalishi nafasi uliyo nayo, wala uzoefu ulio nao, au kiasi unachojua, kama hauna sheria ya wema katika kinywa chako, harufu nzuri ya upendo inayotiririka kutoka katika moyo wako, huwezi kufanya cho chote kama ipasavyo.
Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba, yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake. (1Yohana 4:20, 21)
Mwonekano wa sura yenye ukweli, uaminifu ya dada au kaka au rafiki ikitolewa kwa namna iliyo ya kawaida kabisa, inayo nguvu ya kufungua milango ya mioyo ambayo inahitaji harufu njema ya maneno yenye kufanana na Kristo na mguso rahisi wa roho ya upendo wa Kristo.
Kote kutuzunguka kunasikikika mayowe ya huzuni iliyopo duniani. Kila mahali wako wahitaji na walio taabuni. Ni sisi tunaohitaji kuongoza katika kuwapoza na kurahisisha magumu ya maisha na huzuni zake. Mahitaji ya roho, ni upendo pekee wa Kristo unaoweza kutosheleza. Kama Kristo atakaa ndani yetu, mioyo yetu itajazwa kwa huruma ya kimbingu. Vijito vilivyofungwa vya upendo wa dhati wakufanana na Kristo vitafunguliwa.
Ni utamu kiasi gani ulitiririka kutoka katika uwepo halisi wa Kristo! Roho hiyo hiyo itaonekana kwa watoto Wake. Wale ambao Kristo anakaa ndani yao watazingirwa na uwepo wa kimbingu. Mavazi yao meupe ya usafi yatakuwa harufu yenye manukato kutoka katika bustani ya Bwana. Nyuso zao zitaakisi nuru kutoka Kwake, zikiangaza njia kwa miguu inayojikwaa na iliyochoka.
Maswali ya Kujitathmini:
1.Je, unatamani kujazwa na upendo wa Kristo na kujazwa na huruma kwa ulimwengu unaoangamia?
2.Ni kwa namna gani za kiutendaji unaweza ukashuhudia kwa majirani zako?
Saturday, 16 January 2016
SIKU YA 09:
KRISTO AKIAKISIWA NDANI YA KANISA:
“Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi. (Yohana 17:23)
• Anzeni kipindi chenu cha maombi kwa kumsifu Mungu kwamba Yeye ni furaha, amani na uvumilivu n.k
• Mtukuze Mungu kwamba ameliita kanisa Lake la masalio kuwa nuru kwa ulimwengu.
• Mtukuze Mungu kwamba ataikamilisha kazi aliyoianzisha katika kanisa.
Kuungama na Kudai Ushindi dhidi ya dhambi (kama dakika 5)
• Muombe Mungu akuonyeshe dhambi unazohitaji kuziungama faraghani. Dai ushindi dhidi ya dhambi hizo.
• Muombe Mungu msamaha kwa nyakati ambazo uliruhusu wivu, kushuku au kutafuta makosa kwa ndugu zako ndani ya moyo wako. Omba kwa ajili ya moyo mpya ukijazwa na upendo pamoja na huruma.
Sala na Maombezi
• Muombe Mungu aandae moyo wako kumpokea Roho Mtakatifu.
• Omba kwa ajili ya familia yako ili iunganishwe na kwamba amani na upendo vitawale makanisa yetu.
• Omba ili Mungu atakase kanisa ili wageni wahisi uwepo wa Roho Mtakatifu.
• Omba ili viongozi wa kanisa (mchungaji wako wa mtaa, wachuganji wa konferensi, unioni, divisheni na Makao Makuu ya Kanisa) wafanye kazi kwa upendo, huruma na umoja katika kumaliza kazi waliyopatiwa na Kristo.
• Omba kwa ajili ya umoja kote ulimwenguni katika mikusanyiko ya kikanisa na upekee wa kanisa ukijengwa katika kuheshimu Neno la Mungu, maombi yenye unyenyekevu, nguvu ya Roho Mtakatifu, kuheshimu sera za kanisa zilizopitishwa na kujiingiza kikamilifu katika utume wa kanisa.
• Omba kwa ajili ya unyenyekevu katika maisha yetu ili tuweze kuunganishwa tunapojitoa katika kutii uongozi wa Mungu na mchakato wa kanisa katika kufanya maamuzi ambayo huamuliwa pamoja na kukubali mapendekezo yatakayopitishwa katika ngazi ya Makao Makuu ya Kanisa.
• Omba ili kwamba tuweze kutoa muda wetu zaidi katika mambo ya umiele kupitia kujifunza Biblia na maombi, ili kumruhusu Mungu kuongoza kwa ukamilifu watu wake kulingana na mapenzi Yake na sio mapenzi yetu. Hii itatusaidia kutuweka daima karibu na Mungu na kuruhusu nguvu ya Roho Mtakatifu kugeuza mazoea ya kiulimwengu ambayo huliweka matatani kanisa la Mungu na maisha yetu ya kila siku.
• Utume Katika Miji Mikuu – Omba kwa ajili ya divisheni yetu ya East –Central Africa na miji tuliyochagua kuifanyia kazi huko: Kinshasa, Dar-es-Salaam, Addis Ababa, Kampala, Kananga, Lodwar, Kigali, Lubumbashi, Goma, Magara na Juba. Omba ili ngome imara za shetani zivunjwe, mahusiano pamoja na Kristo yajengwe.
• Omba kwa ajili ya ulinzi kwa vijana na sisi sote kutoka katika mivuto inaoongezeka kila siku ya kidunia. Omba ili tuweze kuweka kipaumbele katika Neno la Mungu na huduma kwa wengine. Omba ili makanisa mahalia yaweze kudhamini vijana katika utume nje ya kanisa na fursa za kutoa huduma.
• Omba ili watu saba au zaidi katika orodha yako waone hitaji la kufungua mioyo yao kwa Roho Mtakatifu.
• Omba kwa ajili ya mahitaji binafsi uliyo nayo.
Shukrani (dakika 10)
• Mshukuru Mungu kwa kile alichofanya katika kanisa Lake na kile atakachokifanya katika kanisa.
• Mshukuru Mungu kwamba yuko tayari kusafisha, kutakasa na kuongoza kanisa.
• Mshukuru Mungu kwamba anafanya kazi katika mioyo ya wale ambao unawaombea.
Mapendekezo ya Nyimbo
Tutajenga juu ya Mwamba no. 72, Msingi wa Kanisa no. 195, Yote Namtolea Yesu no. 122,
KRISTO AKIAKISIWA NDANI YA KANISA
“Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi. Yohana 17:23
Hakuna kitu cho chote ambacho kinaweza kuhafifisha mvuto wa kanisa kama kukosekana kwa upendo….. Watu wa kidunia wanatuangalia ili kuona kile imani inachofanya katika tabia na maisha yetu. Wanaangalia kuona kama imani hiyo ina matokeo ya kuleta utakaso katika mioyo yetu, kama tumebadilishwa kufanana na Kristo. Wako makini kugundua kila dosari katika maisha yetu, kila kukosa msimamo katika matendo yetu, hebu tusiwape nafasi kukebehi imani yetu. Sio upinzani duniani ambao utatuweka hatarini bali ni uovu unaoendekezwa katikati yetu ambao huleta matokeo ya kutisha. Ni maisha ya watu wasiojitoa kikamilifu na kutoa mioyo yao nusu nusu ambayo huzuia kazi ya ukweli na kuleta giza katika kanisa la Mungu.
Hakuna njia yenye uhakika zaidi ya kutufanya tudhoofike katika mambo ya kiroho kama kuwa na wivu, hali ya kushuku, kujawa na kutafuta makosa na kupuuzia dhambi….Unapokuwa pamoja na watu wengine, linda maneno yako…. Kama kuipenda kweli kuko ndani ya moyo wako utaongea ile kweli. Utaongea juu ya tumaini lenye baraka ulilo nalo katika Yesu. Kama una upendo katika moyo wako utatafuta kumuimarisha na kumjenga ndugu yako katika imani iliyo takatifu zaidi. Kama neno litaponyoka katika midomo lenye kuharibu tabia ya rafiki au ndugu yako, usiendekeze uzungumzaji huo mbaya kwani hiyo ni kazi ya adui. Kwa upole mkumbushe mzungumzaji kwamba Neno la Mungu linakataa uzungumzaji wa namna hiyo. Tunapaswa kumimina kiini cha kila kitu ambacho kinalinajisi hekalu ya roho, ili Kristo aweze kukaa ndani. Mwokozi wetu ametuambia namna tunavyoweza kumfunua kwa ulimwengu. Kama tutadumisha Roho Wake, kama tutadhihirisha upendo Wake kwa wengine, kama tutalinda maslahi ya kila mmoja wetu, kama tutakuwa watu wema, wavumilivu, wastahimilivu, ulimwengu utakuwa na ushahidi wa matunda tutakayozaa kwamba sisi tu watoto wa Mungu. Ni umoja katika kanisa ambao huliwezesha kanisa kuufanyia kazi mvuto wenye ufahamu kwa waumini na wakazi wa dunia. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi. Yohana 13:35.
Dini ya Kristo ni zaidi ya msamaha wa dhambi; humaanisha kwamba dhambi zimeondolewa na kwamba sehemu iliyobaki tupu imejazwa na Roho Mtakatifu. Inamaanisha kwamba akili hutiwa nuru ya mbinguni na moyo huondolewa ubinafsi wote na kujazwa na uwepo wa Kristo. Wakati hili linapofanyika kwa washiriki wa kanisa, kanisa litakuwa hai na lenye kufanya kazi. Tutakapoweka mioyo yetu katika umoja na Kristo na maisha yetu yakapatikana na kazi Yake, Roho ambaye alishuka wakati wa Pentekoste atamwagwa kwetu. Tutakuwa imara katika nguvu ya Kristo na kujazwa na ukamilifu wa Mungu……Tutajitoa kwa Kristo, na kuweka wakfu vyote tulivyo navyo, uwezo wetu wote katika huduma ya Kristo. Tutaitangaza imani yetu vyema, tutamtumikia Mungu kwa kuwahudumia wale wanaohitaji msaada wetu. Ndipo tutaruhusu nuru yetu kuangaza kwa matendo mema.
Kama wanafunzi wa Yesu walivyojazwa na nguvu ya Roho Mtakatifu, wakaenda kutangaza injili, hivyo hivyo watumishi wa Mungu wanatakiwa kwenda kutangaza injili. Kila ambaye anamulikiwa na nuru ya ukweli wa leo anapaswa kuamshwa kwa kuwahurumia wale walioko gizani. Kutoka kwa washiriki wote nuru yapaswa kuakisiwa katika mionzi iliyo wazi na ming’aavu. Kazi kama ile ile aliyoifanya Bwana kupitia kwa wajumbe wake baada ya siku ya Pentekoste anasubiri kuifanya hata leo. Katika kipindi hiki, wakati mwisho wa mambo yote umekaribia, ari ya kanisa yapaswa kuzidi ile ya kanisa la awali. Ari kwa ajili ya utukufu wa Mungu iliwafanya wanafunzi kubeba ushuhuda wa ukweli kwa nguvu nyingi. Je ari hii haipaswi kuichoma mioyo yetu kwa ajili ya kuwiwa kuhadithia kisa cha upendo uokoao wa Kristo aliyesulubishwa?
Maswali ya Kujitathmini:
1. Je wewe, mshiriki wa kanisa hai la Kristo, wawezaje kuhimiza umoja na upendo kwa ndugu zako?
2. Tafakari kwa maombi kama unahitaji kusamehe, au kuomba msamaha au kupatana na ye yote ndani au nje ya kanisa.
KRISTO AKIAKISIWA NDANI YA KANISA:
“Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi. (Yohana 17:23)
• Anzeni kipindi chenu cha maombi kwa kumsifu Mungu kwamba Yeye ni furaha, amani na uvumilivu n.k
• Mtukuze Mungu kwamba ameliita kanisa Lake la masalio kuwa nuru kwa ulimwengu.
• Mtukuze Mungu kwamba ataikamilisha kazi aliyoianzisha katika kanisa.
Kuungama na Kudai Ushindi dhidi ya dhambi (kama dakika 5)
• Muombe Mungu akuonyeshe dhambi unazohitaji kuziungama faraghani. Dai ushindi dhidi ya dhambi hizo.
• Muombe Mungu msamaha kwa nyakati ambazo uliruhusu wivu, kushuku au kutafuta makosa kwa ndugu zako ndani ya moyo wako. Omba kwa ajili ya moyo mpya ukijazwa na upendo pamoja na huruma.
Sala na Maombezi
• Muombe Mungu aandae moyo wako kumpokea Roho Mtakatifu.
• Omba kwa ajili ya familia yako ili iunganishwe na kwamba amani na upendo vitawale makanisa yetu.
• Omba ili Mungu atakase kanisa ili wageni wahisi uwepo wa Roho Mtakatifu.
• Omba ili viongozi wa kanisa (mchungaji wako wa mtaa, wachuganji wa konferensi, unioni, divisheni na Makao Makuu ya Kanisa) wafanye kazi kwa upendo, huruma na umoja katika kumaliza kazi waliyopatiwa na Kristo.
• Omba kwa ajili ya umoja kote ulimwenguni katika mikusanyiko ya kikanisa na upekee wa kanisa ukijengwa katika kuheshimu Neno la Mungu, maombi yenye unyenyekevu, nguvu ya Roho Mtakatifu, kuheshimu sera za kanisa zilizopitishwa na kujiingiza kikamilifu katika utume wa kanisa.
• Omba kwa ajili ya unyenyekevu katika maisha yetu ili tuweze kuunganishwa tunapojitoa katika kutii uongozi wa Mungu na mchakato wa kanisa katika kufanya maamuzi ambayo huamuliwa pamoja na kukubali mapendekezo yatakayopitishwa katika ngazi ya Makao Makuu ya Kanisa.
• Omba ili kwamba tuweze kutoa muda wetu zaidi katika mambo ya umiele kupitia kujifunza Biblia na maombi, ili kumruhusu Mungu kuongoza kwa ukamilifu watu wake kulingana na mapenzi Yake na sio mapenzi yetu. Hii itatusaidia kutuweka daima karibu na Mungu na kuruhusu nguvu ya Roho Mtakatifu kugeuza mazoea ya kiulimwengu ambayo huliweka matatani kanisa la Mungu na maisha yetu ya kila siku.
• Utume Katika Miji Mikuu – Omba kwa ajili ya divisheni yetu ya East –Central Africa na miji tuliyochagua kuifanyia kazi huko: Kinshasa, Dar-es-Salaam, Addis Ababa, Kampala, Kananga, Lodwar, Kigali, Lubumbashi, Goma, Magara na Juba. Omba ili ngome imara za shetani zivunjwe, mahusiano pamoja na Kristo yajengwe.
• Omba kwa ajili ya ulinzi kwa vijana na sisi sote kutoka katika mivuto inaoongezeka kila siku ya kidunia. Omba ili tuweze kuweka kipaumbele katika Neno la Mungu na huduma kwa wengine. Omba ili makanisa mahalia yaweze kudhamini vijana katika utume nje ya kanisa na fursa za kutoa huduma.
• Omba ili watu saba au zaidi katika orodha yako waone hitaji la kufungua mioyo yao kwa Roho Mtakatifu.
• Omba kwa ajili ya mahitaji binafsi uliyo nayo.
Shukrani (dakika 10)
• Mshukuru Mungu kwa kile alichofanya katika kanisa Lake na kile atakachokifanya katika kanisa.
• Mshukuru Mungu kwamba yuko tayari kusafisha, kutakasa na kuongoza kanisa.
• Mshukuru Mungu kwamba anafanya kazi katika mioyo ya wale ambao unawaombea.
Mapendekezo ya Nyimbo
Tutajenga juu ya Mwamba no. 72, Msingi wa Kanisa no. 195, Yote Namtolea Yesu no. 122,
KRISTO AKIAKISIWA NDANI YA KANISA
“Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi. Yohana 17:23
Hakuna kitu cho chote ambacho kinaweza kuhafifisha mvuto wa kanisa kama kukosekana kwa upendo….. Watu wa kidunia wanatuangalia ili kuona kile imani inachofanya katika tabia na maisha yetu. Wanaangalia kuona kama imani hiyo ina matokeo ya kuleta utakaso katika mioyo yetu, kama tumebadilishwa kufanana na Kristo. Wako makini kugundua kila dosari katika maisha yetu, kila kukosa msimamo katika matendo yetu, hebu tusiwape nafasi kukebehi imani yetu. Sio upinzani duniani ambao utatuweka hatarini bali ni uovu unaoendekezwa katikati yetu ambao huleta matokeo ya kutisha. Ni maisha ya watu wasiojitoa kikamilifu na kutoa mioyo yao nusu nusu ambayo huzuia kazi ya ukweli na kuleta giza katika kanisa la Mungu.
Hakuna njia yenye uhakika zaidi ya kutufanya tudhoofike katika mambo ya kiroho kama kuwa na wivu, hali ya kushuku, kujawa na kutafuta makosa na kupuuzia dhambi….Unapokuwa pamoja na watu wengine, linda maneno yako…. Kama kuipenda kweli kuko ndani ya moyo wako utaongea ile kweli. Utaongea juu ya tumaini lenye baraka ulilo nalo katika Yesu. Kama una upendo katika moyo wako utatafuta kumuimarisha na kumjenga ndugu yako katika imani iliyo takatifu zaidi. Kama neno litaponyoka katika midomo lenye kuharibu tabia ya rafiki au ndugu yako, usiendekeze uzungumzaji huo mbaya kwani hiyo ni kazi ya adui. Kwa upole mkumbushe mzungumzaji kwamba Neno la Mungu linakataa uzungumzaji wa namna hiyo. Tunapaswa kumimina kiini cha kila kitu ambacho kinalinajisi hekalu ya roho, ili Kristo aweze kukaa ndani. Mwokozi wetu ametuambia namna tunavyoweza kumfunua kwa ulimwengu. Kama tutadumisha Roho Wake, kama tutadhihirisha upendo Wake kwa wengine, kama tutalinda maslahi ya kila mmoja wetu, kama tutakuwa watu wema, wavumilivu, wastahimilivu, ulimwengu utakuwa na ushahidi wa matunda tutakayozaa kwamba sisi tu watoto wa Mungu. Ni umoja katika kanisa ambao huliwezesha kanisa kuufanyia kazi mvuto wenye ufahamu kwa waumini na wakazi wa dunia. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi. Yohana 13:35.
Dini ya Kristo ni zaidi ya msamaha wa dhambi; humaanisha kwamba dhambi zimeondolewa na kwamba sehemu iliyobaki tupu imejazwa na Roho Mtakatifu. Inamaanisha kwamba akili hutiwa nuru ya mbinguni na moyo huondolewa ubinafsi wote na kujazwa na uwepo wa Kristo. Wakati hili linapofanyika kwa washiriki wa kanisa, kanisa litakuwa hai na lenye kufanya kazi. Tutakapoweka mioyo yetu katika umoja na Kristo na maisha yetu yakapatikana na kazi Yake, Roho ambaye alishuka wakati wa Pentekoste atamwagwa kwetu. Tutakuwa imara katika nguvu ya Kristo na kujazwa na ukamilifu wa Mungu……Tutajitoa kwa Kristo, na kuweka wakfu vyote tulivyo navyo, uwezo wetu wote katika huduma ya Kristo. Tutaitangaza imani yetu vyema, tutamtumikia Mungu kwa kuwahudumia wale wanaohitaji msaada wetu. Ndipo tutaruhusu nuru yetu kuangaza kwa matendo mema.
Kama wanafunzi wa Yesu walivyojazwa na nguvu ya Roho Mtakatifu, wakaenda kutangaza injili, hivyo hivyo watumishi wa Mungu wanatakiwa kwenda kutangaza injili. Kila ambaye anamulikiwa na nuru ya ukweli wa leo anapaswa kuamshwa kwa kuwahurumia wale walioko gizani. Kutoka kwa washiriki wote nuru yapaswa kuakisiwa katika mionzi iliyo wazi na ming’aavu. Kazi kama ile ile aliyoifanya Bwana kupitia kwa wajumbe wake baada ya siku ya Pentekoste anasubiri kuifanya hata leo. Katika kipindi hiki, wakati mwisho wa mambo yote umekaribia, ari ya kanisa yapaswa kuzidi ile ya kanisa la awali. Ari kwa ajili ya utukufu wa Mungu iliwafanya wanafunzi kubeba ushuhuda wa ukweli kwa nguvu nyingi. Je ari hii haipaswi kuichoma mioyo yetu kwa ajili ya kuwiwa kuhadithia kisa cha upendo uokoao wa Kristo aliyesulubishwa?
Maswali ya Kujitathmini:
1. Je wewe, mshiriki wa kanisa hai la Kristo, wawezaje kuhimiza umoja na upendo kwa ndugu zako?
2. Tafakari kwa maombi kama unahitaji kusamehe, au kuomba msamaha au kupatana na ye yote ndani au nje ya kanisa.
Wednesday, 13 January 2016
SIKU YA – 8:
KRISTO AKIAKISIWA KATIKA FAMILIA:
“Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.” 1Yohana 4:7
Mapendekezo ya Utaratibu wa Kipindi cha Maombi
Kusifu (takribani dakika 10)
Anzeni kipindi cha maombi kwa kumsifu Mungu kwa jinsi alivyo (Tabia Yake). Yeye ni mwenye neema n.k
Msifu Mungu kwamba Yeye ni Baba wa familia ya wanadamu duniani.
Msifu Mungu kwamba anataka familia ya kibinadamu iakisi uzuri Wake na tabia Yake.
Kuungama na Kudai Ushindi dhidi ya dhambi
Muombe Mungu akuonyeshe dhambi unazohitaji kuziungama kwa siri. Dai ushindi juu ya dhambi hizo.
Muombe Mungu msamaha kwa nyakati ambazo hukumuakisi Mungu katika familia yako.
Muombe Mungu msamaha kwa nyakati ambazo hukuwaheshimu na kuwatii wazazi wako pamoja na ndugu mliozaliwa nao.
Mshukuru Mungu kwamba anakusamehe kulingana na 1Yohana 1:9.
Sala na Maombezi
Muombe Mungu ajaze moyo wako kwa Roho Mtakatifu na kukufanya kuwa mfano hai kwa familia yako
Muombe Mungu ili kila mwanafamilia katika famila yako avutwe karibu na Kristo
Muombe Mungu azilinde familia za Kiadventista dhidi ya mashambulio ya Shetani, zikiwemo familia katika kanisa lako mahalia. Muombe Mungu kwa ajili ya uponyaji pale inapohitajika.
Omba ili kwamba viongozi wa kanisa (mchungaji wako wa mtaa, wachungaji wa konferensi, unioni, divisheni na Makao Makuu ya Kanisa) pamoja na familia zao wamuakisi Kristo kwa ulimwengu.
Omba kwa ajili ya mavuno ya pekee ya roho kutokana na mbegu zilizopandwa wakati wa mradi wa usambazaji wa kitabu cha Tumaini Kuu katika mifumo yake yote.
Omba kwamba wazazi wamuakisi Kristo kwa watoto wao na kuwalea kwa ajili ya Ufalme.
Omba ili kwamba Mungu alete uelewa kamili wa njia aliyoitumia Kristo (huduma kamili ya uponyaji) ili kwamba washiriki wote wasaidie watu kwa kuwapatia mahitaji yao na kufuata kilelezo cha Kristo katika kuhudumia wengine.
Omba kwa ajili ya muunganiko wa harakati za uinjilisti na ushuhudiaji wa kila mwanaume, mwanamke na watoto wote wa Kiadventista kote duniani. Omba kwamba tujazwe na Roho Mtakatifu tunapojisalimisha kwa uongozi wake katika maisha yetu.
Msihi Bwana kwa niaba ya familia za Kiadventista ili ziwe kielelezo cha jinsi Kristo anavyoweza kuleta amani na upendo majumbani, kuondoa kila unyanyasaji na misongo kupitia kwa nguvu itakasayo ya haki ya Kristo na kuelekeza watu kwa kuja kwa Kristo kuliko karibu na hatimae kuungana na familia ya milele ya Mungu huko mbinguni.
Utume katika Miji Mikuu Omba kwa ajili ya Divisheni ya Euro-Asia na miji wanayoifanyia kazi: Moscow, Kiev, Kishinev, Donetsk, Kharkov, Minsk, St. Petersburg, Novosibirsk, Krasnoyarsk, Khabarovsk, Rostov -on-Don, Tbilisi, Yerevan na Almaty. Omba kwa ajili ya maelfu ya huduma za kuwafikia watu na matukio yanayoendelea ya uvunaji wa roho.
Omba ili kwamba watu saba au zaidi katika orodha yako waone hitaji lao na kufungua mioyo yao kwa Roho Mtakatifu.
Omba kwa ajili ya mahitaji binafsi uliyo nayo.
Shukrani (dakika 10)
Mshukuru Mungu kwamba anafanyia kazi mioyo ya wanafamilia wako.
Mshukuru Mungu kwamba yu tayari kukusafisha, kukutakasa na kukaa ndani yako na ndani ya familia yako.
Mshukuru Mungu kwamba Yesu ametupatia kielelezo cha jinsi ya kuwaheshimu wazazi wetu pamoja na kuwapenda ndugu tuliozaliwa nao.
Mapendekezo ya Nyimbo
Kuwa na Yesu Nyumbani no. 204, Panapo Pendo no.184, Upendo ni Furaha no. 199
KRISTO AKIAKISIWA KATIKA FAMILIA:
“Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.” 1Yohana 4:7
Dini ya Kristo itatuongoza katika kufanya mambo yote mema kadiri iwezekanavyo, kwa watu wa daraja la juu na la chini, kwa matajiri na maskini, kwa wenye furaha na wale wanaoonewa. Lakini haswa itatuongoza katika udhihirisho wa wema katika familia zetu wenyewe. Dini hiyo itadhihirika katika matendo ya adabu, na upendo kwa baba, mama, mke na mtoto. Tunapaswa tumwangalie Yesu, kukamata roho Yake, kuishi katika nuru ya wema Wake na upendo na kuakisi utukufu Wake kwa wengine.
“Basi mtiini Mungu, Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.” Yakobo 4:7
Kama utajitoa kikamilifu kwa Yesu, ataumba ndani yako tamanio la kina kwa ajili ya urafiki na Mungu, nawe utajazwa shauku ya kuakisi wema Wake na upendo Wake katika maisha yako na tabia yako kwa familia yako na kwa wale wasioufahamu upendo Wake. Kwa kupanda uvumilivu, upole, ustahimilivu, kwa kuonyesha heshima na kuwapa utii mama yako na baba yako kama impendezavyo Bwana, utakuwa ukitoa ushuhuda katika maisha yako ya kila siku kwamba ukweli una nguvu ya kutakasa tabia.
Ni swala gumu kurekebisha mambo magumu katika familia, hata pale ambapo mume na mke wanatafuta kufanya hivyo kama wameshindwa kusalimisha mioyo yao kwa Mungu.
Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake. Yohana 7:38.
Kama mapenzi ya Mungu yatatimizwa, mume na mke wataheshimiana na kuotesha upendo na ujasiri. Cho chote kile ambacho chaweza kuharibu amani na umoja wa familia chapaswa kuzuiwa kwa uthabiti na utu wema pamoja na upendo vyapaswa kudumishwa. Mtu yule ambaye anadhihirisha roho ya upole, ustahimilivu na upendo atagundua kuwa roho ile ile itaakisiwa toka kwake. Mahali ambapo Roho wa Mungu anatawala, hakutakuwa na maongezi yasiyofaa katika mahusiano ya ndoa. Kama kweli Kristo atajengwa ndani kwa kina, tumaini la utukufu, kutakuwa na umoja na upendo nyumbani. Kristo akikaa katika moyo wa mke kutakuwa na makubaliano pamoja na Kristo anayekaa ndani ya moyo wa mume. Watafanya bidii pamoja kwa ajili ya kwenda katika makao ambayo Kristo amekwenda kuandaa kwa wale wampendao.
Lazima tuwe na Roho wa Mungu, au kamwe hatutakuwa na mwafaka nyumbani. Mke, kama ana roho wa Kristo atakuwa makini na maneno yake, atajizuia, atakuwa mtii na bado hatajisikia kana kwamba ni mtumwa, lakini mwenzi wa mumewe. Kama mume ni mtumishi wa Mungu, hatamtawala mke wake, hatakuwa dikteta na mkali. Hatutaweza kudumisha upendo nyumbani kwa kuwa waangalifu kupita kiasi, kwani Roho wa Bwana akiwepo nyumbani, panakuwa sehemu ya mbinguni……mmoja anapokosea, mwingine atafanyia mazoezi ustahimilivu kama wa Kristo badala ya kumpa kisogo mwenzake na kuondoka.
Kama unayo matazamio makubwa na kusudi la kufika katika kiwango cha juu, maisha ya nyumbani yanaweza kukupa adabu bora zaidi. Kama ukikosea nyumbani, utakosa katika kila lengo na kila jitihada. Anza nyumbani ili kukamilisha tabia ambayo Mungu ataikubali, tabia itakayofanya uwe mbaraka nyumbani, na utakapokuwa mbali na nyumbani, hautashindwa kuwa mbaraka kwa wale utakaokutana nao. Dini inayofanyiwa mazoezi nyumbani huakisi mbali zaidi ya wigo wa hapo nyumbani.
Maswali ya Kujitathmini:
1.Je unawezaje kuongoza familia yako kwa kielelezo cha maisha tele kwa Kristo?
2.Je daima umekuwa mwanafamilia mzuri? Je kuna mambo ambayo unahitaji kurekebisha? Je wahitaji kuifanya familia yako kuwa kipaumbele zaidi ya mambo mengine?
SIKU YA – 7:
MAISHA AMBAYO HUBARIKI WENGINE:
“Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake. Yohana 7:38
Mapendekezo ya utaratibu wa maombi Kusifu (dakika 10) Anzeni kipindi chenu cha maombi kwa kumsifu Mungu kwa jinsi aliyo (tabia Yake). Yeye ni Mungu wa milele, Mungu mvumilivu na mwenye upendo. Mungu ndiye nguvu yetu (Zaburi 27:1) na Yeye ndiye mahali petu pa kupumzika. (Yeremia 50:6). Mtukuze Mungu kwa utayali wake wa kututumia kubariki wengine, hata kama tuna mapungufu na makosa. Mtukuze Mungu kwamba sio sisi ambao tunagusa na kubariki maisha ya watu bali ni Kristo ndani yetu Kuungama na Kudai Ushindi dhidi ya dhambi Muombe Mungu akuonyeshe dhambi utakazoziungama hadharani na zile za kuungama faraghani. Dai ushindi Wake dhidi ya dhambi hizo. Muombe Mungu akusamehe katika nyakati ambazo maisha yako hayakuwa mbaraka kwa wengine. Muombe Mungu msamaha katika nyakati ambazo ulijali zaidi mafaniko yako kuliko kumtumikia Yeye. Mshukuru Mungu kwamba anakusamehe kulingana 1Yohana 1:9. Sala na
Maombezi Mwombe Mungu akupe imani hata pale ambapo shetani hujaribu kukukatisha tamaa usiwahudumie wengine. Muombe Mungu akupe mzigo wa roho za watu wengine na upendo kwa watoto wa Mungu waliopotea. Omba kwa ajili ya tabia inayopendeza, tabia ya kufanana na Kristo itakayowavuta watu kwa Yesu. Omba kwa ajili ya kila mshiriki kuhisi mzigo wa kuongoa roho na kutambua kwamba mbingu inamhitaji kila mmoja kufuata kielelezo cha Kristo kwa kushiriki imani yake akiongozwa na Mungu. Omba kwa ajili ya kutumia vyanzo vyote vya habari vitakavyofaa katika kushiriki ujumbe wa malaika wa tatu katika namna mpya na yenye ubunifu kwa watu wenye shughuli nyingi wa siku hizi. Omba ili idadi iongozeke ya washiriki wote na kujiunga na uinjilisti na taasisi wanapounga mkono utume wa kanisa unaoendelea.
Utume katika Miji Mikuu - Omba kwa ajili ya Divisheni ya Inter-American na miji wanayotamani kuileta kwa Kristo: Mexico, Caracas, Bogatá, Nassau, Belize, Georgetown, Cali, Cayenne, Guatemala, Quetzaltenango, Port-au-Prince, Tegucigalpla, Mérida, kisiwa chote cha Puerto Rico. Santiago de los Caballeros na Maracaibo. Omba ili washiriki waendeleze mikakati ya kufikia miji mikubwa. Omba juu ya kuanzishwa kwa maelfu ya “vyanzo vya vivutio” (makanisa, vituo vya afya, shule za kutwa, mahali vitabu vinapouzwa, vituo vya kuhudumia jamii, vikundi vya vijana, migahawa ya vyakula visivyo na nyama, zahanati na mengineyo) haswa katika miji mikubwa duniani, omba pia vituo hivi vifanye tofauti kubwa katika maisha ya watu wanapopata uzoefu wa ukweli wa Mungu kupitia huduma ya Kikristo. Omba ili kwamba watu saba au zaidi katika orodha yako waone hitaji lao na kufungua mioyo yao kwa Roho Mtakatifu. Omba kwa ajili ya mahitaji binafsi uliyo nayo.
Shukrani (takribani dakika 10) Mshukuru Mungu kwamba anataka kututumia sisi wala sio malaika kuwa watendakazi pamoja Naye kubariki wengine. Mshukuru Mungu kwamba Yesu ametupatia kielelezo cha jinsi ya kuwa mbaraka kwa watu wengine. Mshukuru Mungu kwamba anatuma Roho wake Mtakatifu kufanya kazi katika mioyo ya wale unaowaombea.
Mapendekezo ya Nyimbo: Popote Mashamba Yajaa no. 94
MAISHA AMBAYO HUBARIKI WENGINE
Kila mtu ambaye Kristo anakaa ndani yake, kila ambaye ataonyesha upendo Wake kwa ulimwengu, ni mtendakazi pamoja na Mungu kwa ajili ya kubariki wanadamu wengine. Kadiri mtu huyo anapopokea kutoka kwa Mwokozi neema ya kuwapatia wengine, kutoka katika utu wake wote kunatiririka wimbi la maisha ya kiroho.
Mwanafunzi wa Yesu aliye mnyenyekevu na maskini zaidi anaweza kuwa mbaraka kwa wengine. Watu kama hao wanaweza wasitambue kama wanafanya jema lo lote, lakini kwa mvuto wao bila kutambua wanaweza wakaanzisha mawimbi ya mibaraka ambayo itapanuka na kuzama chini, na matokeo yenye baraka wanaweza wasiyajue hadi wakati wa thawabu ya mwisho. Watu hao hawajisikii wala hawajui kama wanafanya jambo lililo kuu, hawahitaji kujichosha kwa wasiwasi wa kupata mafanikio. Wanahitaji tu kwenda mbele kimya, wakifanya kwa uaminifu kazi ambayo uongozi wa Mungu unaagiza, na maisha yao hayatakuwa bure. Roho zao wenyewe zitakuwa zikikua zaidi na zaidi katika kufanana na Kristo; wao ni watendakazi pamoja na Mungu katika maisha haya, na hivyo wanastahili kazi iliyo bora zaidi na furaha isiyo na kivuli ya maisha yajayo.
Bwana anatuita tuamke katika kutambua wajibu wetu. Mungu amempatia kika mwanadamu kazi yake, hivyo kila mmoja anaweza kuishi maisha yenye manufaa. Hebu tujifunze yote tuwezayo na hatimae tuwe mbaraka kwa wengine kwa kuwapatia maarifa ya ukweli. Hebu kila mmoja atende kwa uwezo wake wote, kwa mamnbo mabalimbali kwa hiari akisaidia wengine kubeba mizigo.
“Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli.”
Waweza kuwa mbaraka mkubwa kwa wengine kama utajitoa mwenyewe kikamilifu kwa ajili ya huduma ya Bwana. Utapewa nguvu kutoka juu kama utasimama upande wa Bwana. Kupitia Kristo unaweza kuepuka ufisadi ulioko duniani katika tamaa na kuwa kielelezo cha uadilifu wa kile ambacho Kristo anaweza kufanya kwa wale wanaoshirikiana Naye. Mungu anatamani wanaume kwa wanawake kuishi maisha yaliyo bora.
Mungu anawapatia wanadamu mafanikio ya maisha, si kwa sababu tu ya kupata tu utajiri, bali kuboresha uwezo wao wa juu kwa kufanya kazi ambayo amewakabidhi wanadamu – kazi ya kutafuta kujua na kuleta nafuu kwa mahitaji ya msingi ya wanadamu wenzao. Mtu anapaswa kufanya kazi si kwa manufaa yake binafsi lakini kwa manufaa ya kila anayemzunguka, akiwabariki wengine kwa mvuto wake na matendo mema. Makusudi haya ya Mungu hudhihirika katika maisha ya Yesu., “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu”. Yakobo 4:6.
Tunapokuwa wanyenyekevu na kusimama tukiwa na hisia za toba tunajiweka mahali ambapo Mungu anaweza na atajifunua mwenyewe kwetu. Yeye hupendezwa sana pale ambapo tunapodai rehema na mibaraka tuliyopewa kipindi kilichopita kama sababu ya Yeye kutumwagia mibaraka mikubwa zaidi. Mungu atatimiza zaidi ya matarajio ya wale ambao wanamtumainia Yeye kikamilifu. Bwana wetu Yesu Kristo anajua kile hasa watoto wake wanachohitaji, na uweza wa uungu kiasi gani ambayo utahitajika kwa mbaraka wa wanadamu; na anatupatia yote ambayo tutahitaji katika kubariki wengine na kuinua roho zetu sisi wenyewe.
Wale ambao wanampenda Mungu kwa dhati watatamani vivyo hivyo kuboresha talanta ambazo amewapatia, ili waweze kuwa mbaraka kwa wengine, na siku kwa siku milango ya mbinguni itafunguliwa wazi kabisa ili kuwaruhusu waingie na kutoka katika mdomo wa Mfalme wa Utukufu baraka zitaanguka katika masikio yao kama muziki wenye nguvu, “Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa kwa ulimwengu.” Mathayo 25:34
Maswali ya Kujitathmini:
1. Ni mambo gani madogo unayoweza kufanya ili yawe mbaraka kwa wale wanaokuzunguka?
2. Mara nyingi ni rahisi kuwa mbaraka kwa watu walio mbali kuliko kwa familia yako. Je wawezaje kuwa mbaraka kwa wale walio karibu nawe?
SIKU YA – 6:
FURAHA YA UTII:
Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako, ambayo nimeyapenda. Zaburi 119:47
Mapendekezo ya utaratibu wa maombi
Kusifu (dakika 10)
Anzeni kipindi chenu cha maombi kwa kumsifu Mungu kwa jinsi alivyo (Tabia Yake), Yeye ni yote katika yote, mfariji, Mhuishaji n.k
Mshukuru Mungu kwa ajili ya Yesu, ambaye ametuonyesha maana ya kuwa na furaha ya utii.
Mshukuru Mungu kwamba kuna shangwe, amani na furaha katika kumtii Kristo.
Kuungamana na Kudai Ushindi dhidi ya dhambi (dakika 5)
Muombe Mungu akuonyeshe dhambi unazohitaji kuziungama faraghani, dai ushindi dhidi ya dhambi hizo.
Mshukuru Mungu kwamba anakusamehe kulingana na 1Yohana 1:9.
Sala na Maombezi (dakika 35)
Je unayo furaha katika kutenda yale Mungu anayokuagiza? Omba kwamba Mungu akupe uhiari wa kumtii Yeye na furaha katika kufanya cho chote anachoagiza.
Omba ili kwamba upendo wa Mungu uweze kukamilishwa katika kanisa Lake.
Omba kwa ajili ya mkazo zaidi katika fundisho la kipekee la uumbaji katika Biblia – kwamba dunia yetu iliumbwa kwa siku halisi sita, zinazofuatana kwa neno la Mungu.
Omba kwa ajili ya ongezeko kubwa katika utegemezaji wa vijana wa Kiadventista ambao wanasoma katika shule za umma. Omba kwamba vijana hao waweze kuwa wamishenari wenye nguvu ambao watahudumia vijana wenzao katika vyuo vya kawaida na vyuo vikuu vya kiserikali.
Omba kwa ajili ya ushirikiano wenye nguvu na umoja katika mfumo wa kanisa na huduma za kanisa zinazounga mkono uinjilisti katika jamii.
Msihi Bwana aweze kulea na kujipatia viongozi wacha Mungu, wanaokuwa tayari kufundishwa na wanyenyekevu kwa ajili ya kipindi kijacho, viongozi ambao wataonyesha mfano wa uongozi ambao kiini chake ni Kristo, wakati kanisa la Mungu linapotimiza wajibu wake toka mbinguni wa kutangaza ujumbe wa malaika wa tatu na haki ya Kristo kama msingi Wake.
Utume katika Majiji – Omba kwa ajili ya Divisheni ya Amerika ya Kaskazini: New York, Calgary, Indianapolis, St. Louis, Seattle, San Francisco, Oakland, Tampa, jiji la Oklahoma. Omba pia kwa ajili ya Divisheni ya Northern Asia-Pacific na miji wanayokusudia kuifikia: Tokyo, Daegu, Daejon, Wuxi, Ulaanbaatar, Taipei. Omba kwa ajili ya Roho wa Mungu kufanya kazi kwa nguvu katika miji hii.
Omba ili washiriki wa kanisa na jamii waelewe umuhimu wa matengenezo ya afya kama sehemu ya kilio kikuu kuwarejesha wanadamu katika sura ya Mungu kupitia kwa haki ya Kristo. Omba kwamba watu wote waweze kuukubali mtindo wa maisha wenye afya na kiasi na kwamba miili yetu itunzwe kama mahekalu ya Roho Mtakatifu, ili kutusaidia kupokea maono muhimu kutoka kwa Mungu.
Omba ili kwamba watu saba au zaidi katika orodha yako waweze kuona hitaji lao na kufungua mioyo yao kwa Roho Mtakatifu.
Omba kwa ajili ya mahitaji yako binafsi. Shukrani
Mshukuru Mungu kwamba kupitia Kristo waweza kusema, kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu (Zaburi 40:8).
Mshukuru Mungu kwamba anao watu wake katika kila mji ambao wanaotazama mbinguni kwa shauku kubwa!
Mshukuru Mungu kwamba anainua viongozi wacha Mungu, wanyenyekevu na walio tayari kufundishwa kwa ajili ya wakati ujao.
Mapendekezo ya Nyimbo
Namwandama Bwana no. 128, Yesu Mwokozi kwa Hakika no. 51, Ni salama Rohoni Mwangu no.127, Mwanga Umo Moyoni no. 45
FURAHA YA UTII
Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako, ambayo nimeyapenda. Zaburi 119:47
Bwana amekusudia kwamba kila roho inayotii neno Lake itakuwa na Furaha Yake, amani Yake, na nguvu yake inayodumu katika kutunza. Wanaume na wanawake watiio kama hao daima huvutwa karibu Naye, si wakati tu wanapopiga magoti kuomba, bali wakati hata wakiendelea na shughuli zao za maisha. Mungu ameandaa kwa ajili yao sehemu ya kukaa ndani Yake, mahali ambapo maisha hutakaswa toka katika uchafu wote na machukizo yote. Kwa ushirika huu pamoja Naye, wanafanywa watendakazi pamoja Naye katika maisha yao yote.
Kristo anapokaa ndani ya moyo, roho itajazwa na upendo Wake, na kwa sababu ya furaha ya ushirika pamoja Naye, ambayo itachoma moyo wake na katika kumtafakari Yeye, ubinafsi utasahauliwa. Upendo kwa Kristo utakuwa sababu ya utendaji. Wale ambao wanaohisi upendo wenye nguvu wa Mungu, hawaulizi ni kiasi gani kidogo kinachoweza kutolewa ili kutimiza matakwa ya Mungu; hawaulizii viwango vya chini, lakini hulenga katika uliganifu kamili wa nia ya Mwokozi wao. Wakiwa na shauku ya dhati hutii yote na kudhihirisha faida linganifu na thamani ya jambo lile wanalolitafuta.
Ni roho ile yenye utii, yenye kukubali mafundisho ambayo Mungu huitaka. Kile kinachofanya ombi liwe bora ni ukweli kwamba linatoka katika moyo wenye upendo na utii.
Mkinipenda mtazishika amri zangu. (Yohana 14:15).
Mtu yule ambaye anajaribu kuzishika amri za Mungu kutokana na kutii wajibu tu, kwa sababu anahitajika kufanya hivyo –kamwe hataingia katika furaha ya utii, kwani hatii. Wakati matakwa ya Mungu yanapohesabiwa kuwa mzigo, kwa sababu yanapingana na mazoea ya kibinadamu, tunaweza kutambua kwamba maisha hayo si maisha ya Kikristo. Utii wa kweli ni matokeo ya kanuni ambayo imo ndani. Hutiririka kutoka katika upendo wa haki, upendo kwa sheria ya Mungu. Kiini cha haki yote ni uaminifu kwa Mwokozi wetu. Hii itatuongoza katika kufanya mambo sahihi kwa sababu mambo hayo ni sahihi – kwa sababu kufanya mambo sahihi ni kumpendeza Mungu.
Tuko katika dunia hii ili tuwe msaada na mbaraka kwa kila mmoja wetu, tukiunganishwa na Kristo katika juhudi ya kurejesha sura ya Mungu kwa mwanadamu. Ili kufanya kazi hii, ni lazima tujifunze kutoka kwa Yesu. “Jitieni nira yangu,” anasema “mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo: nanyi mtapata raha nafsini mwenu.” Katika ahadi hii hakuna “kama”. Wale ambao wamepata uzoefu wa kujitia nira ya Kristo ya kujitawala na utii wanajua kwamba inamaanisha kupata pumziko na amani katika Yeye. Katika utii kuna furaha na farijiko. Malaika watakatifu huwazingira watiifu ili kuwatunza katika njia za amani.
Hakuna imani iokoayo katika Kristo pekee kama ambayo inadhihirishwa katika utii. Kila mwanadamu yupo chini ya wajibu mkubwa wa kumtii Mungu. Uwepo wa Mungu na furaha ya milele inategemea na utii wa hiari wa mtu kwa matakwa ya mbingu. Nia ya mtu na matakwa yake yapaswa yasalimishwe kwa Mungu. Wakati hilo linapofanyika, mtu atashirikiana na Mungu akionyesha kwa mwenendo na kwa kielelezo kuwa amechagua kuwa chini ya utawala wa Muumbaji wake katika njia zake zote. Mungu anafurahi wakati ambapo, kama Musa, watoto wake wanaamua kuchagua kumtumikia Yeye badala ya kufarahia anasa za dunia hii. Kama pazia lingeweza kufunuliwa, kama wanadamu wangeweza kuona jeshi la malaika wakimtukuza Mungu kwa nyimbo za shangwe na furaha, wangetambua kwamba utii daima huleta furaha na kutokutii huleta huzuni. Mungu na malaika hushangilia juu ya kila ushindi apatao Mkristo; lakini jaribu linapoishinda nafsi, kunakuwepo huzuni mbinguni.
Tunaupeleka uongo kwenye ukweli na kumtukuza shetani pale ambapo tunatembea tukiwa na huzuni na majonzi kwa sababu tunadhani kwamba matakwa yanayohitajika kwetu katika maisha ya Kikristo ni mengi kuliko vile tuwezavyo. Mkombozi wako anakupenda, na anakupatia furaha za umilele katika maisha ya utii. Hakuna ambaye amewahi kuonja furaha ya utii mkamilifu na wa hiari kwa Mungu, ambaye hakupata amani, furaha na uthibitisho wa pendo Lake.
Maswali ya Kujitathmini:
Je unapitia uzoefu wa utii kwa Kristo?
Je kuna jambo lo lote linalokuzuia kupata furaha katika kumtii Mwokozi wako mpendwa?
SIKU YA – 5:
ZAIDI YA KUSHINDA:
“Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.” Wakorintho 8:37.
Kusifu (takribani dakika 10) Anzeni kipindi cha maombi kwa kumsifu Mungu kwa jinsi alivyo yaani tabia Yake. Msifuni kwa uaminifu Wake na kwamba Yeye ni kimbilio. Msifu Mungu kwamba yote unayotakiwa kufanya ni kukaa ndani ya Kristo ili upate ushindi dhidi ya dhambi. Msifu Mungu kwamba Yesu alipata ushindi dhidi ya dhambi pale msalabani. Kuungama na Kudai Ushindi dhidi ya Dhambi (dk5) Muombe Mungu akuonyeshe dhambi ambazo unahitaji kuziungama kwa uwazi na zile ambazo unahitaji kuziungama faraghani. Dai ushindi dhidi ya dhambi hizo. Je kumekuwepo na nyakati ambazo hukujisikia kwamba ulitaka kuishinda dhambi? Muombe Mungu msamaha. Muombe Mungu aweke tamanio ndani ya moyo wako la kuishinda dhambi. Muombe Mungu msamaha kwamba sisi, kama kanisa bado hatujaweza kuishinda dhambi. Mshukuru Mungu kwamba anakusamehe kulingana na 1 Yohana 1:9. Sala na Maombezi (dakika 35) Omba kwamba Mungu akupe tamanio la kuishinda dhambi. Ombea wanafamilia na marafiki ambao pia wanahitaji kupata ushindi dhidi ya dhambi. Ombea mahali ambapo katika maisha yako bado unahitaji kupata ushindi dhidi ya dhambi. Muombe Mungu akupe ushindi kamili. Muombe Mungu akusaidie uamini kwamba Yeye anaweza kukupatia ushindi kamili dhidi ya dhambi. Je bado unashikilia sanamu katika maisha yako? Zilete sanamu hizo mbele za Mungu na muombe akupe chuki moyoni mwako dhidhi ya sanamu hizo.
Omba ili viongozi wa kanisa (Mchungaiji wako wa mtaa, wachungaji wa konferensi, unioni, divisheni na Makao Makuu ya Kanisa) wamruhusu Mungu awape ushindi dhidi ya dhambi.
Omba ili Mungu akufanye uwe mnyenyekevu ili uweze kuona udhaifu wako na kuomba nguvu ya kushicnda udhaifu huo.
Omba kwa ajili ya mipango mikubwa ya uinjilisti na huduma nje ya kanisa katika divisheni zote 13 pamoja na unioni moja iliyo pamoja na divisheni hizo, unioni ya (Middle East and North Africa Union).
Omba kwa ajili ya mafanikio katika “Utume Katika Majiji” na katika kufikia maeneo ya vijijini. Utume katika Miji Mikubwa –
Omba kwa ajili ya divisheni ya South America na miji 74 ambayo wameichagua ili kuihudumia. Omba pia kwa ajili ya Divisheni ya Pasifiki ya Kusini na miji ambayo wameichagua kuifikia kwa ajili Kristo: miji hiyo ni Sydney, Christchurch, Lae, Apia.
Omba ili kwamba Mungu atume watenda kazi na aweze kubariki jitihada zao.
Omba ili Mungu aendelee kuongoza kanisa Lake na kuwapa washiriki ushindi dhidi ya dhambi. Omba ili watu saba (au zaidi) katika orodha yako waweze kuona hitaji lao na kufungua mioyo yao kwa Roho Mtakatifu.
Omba kwa ajili ya mahitaji yako binafsi uliyo nayo (Mithali 3:5, 6).
Shukrani (takribani dakika 10) Mshukuru Mungu kwamba yupo radhi kukupatia haki Yake. Mshukuru Mungu kwamba Yeye ndiye “Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.” Wafilipi 2:13 Mshukuru Mungu kwa ajili ya maisha ya Yesu yasiyo na dhambi na jinsi ambavyo ametuonyesha jinsi ya kuwa washindi. Mshukuru Mungu kwamba anajibu maombi uliyoomba kulingana na mapenzi Yake.
Mapendekezo ya Nyimbo: Si Mimi Kristo no. 17, Usinipite Mwokozi no.22, Mtazame Mwokozi no.212, Mwamba Wenye Imara no. 192
ZAIDI YA KUSHINDA.
“Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.” Wakorintho 8:37
Katika pambano lao na Shetani, familia ya kibinadamu inao msaada wote aliokuwa nao Kristo. Hawatakiwi kushindwa. Wanaweza kuwa zaidi ya washindi kupitia Yeye ambaye aliwapenda na akatoa maisha Yake kwa ajili yao….Mwana wa Mungu katika ubinadamu Wake alipambana na hali mbaya vivyo hivyo, majaribu mazito ambayo hutushambulia – majaribu ya uchu wa chakula, kuwa na kiburi kuthubutu kuenenda mahali ambapo Mungu hajaongoza na kuelekea katika kumuabudu mungu wa ulimwengu huu, kutoa mhanga umilele wa mbinguni kwa anasa zinazovutia za ulimwengu huu. Kila mmoja atajaribiwa, lakini Neno linasema kwamba hatutajiribiwa kupita tuwezavyo kuvumilia. Tunaweza hata hivyo kukataa na kumshinda adui mwenye hila. Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili. (1Wakorintho 10:13)
Kazi yetu ya katika maisha tuliyopewa ni kazi ya maandalizi ya maisha ya umilele, na tutakapokamilisha kazi hii kama Mungu alivyowezesha tuifanye, kila jaribu litakuwa kwa kutufanya tusonge mbele; kwani tutakapokataa kuhadaika na jaribu hilo tutasonga mbele katika maisha ya kimbingu. Katika joto la pambano, wakati tunapojihusisha kikamilifu katika vita ya kiroho, mawakala wasioonekana kwa macho wako kando yetu, waliokabidhiwa mamlaka na mbingu kutuongoza katika mapambano yetu na wakati wa hatari, tunapatiwa nguvu, uthabiti na uwezo, na tunakuwa na nguvu zaidi ya ile ya kibinadamu.Lakini isipokuwa pale tu wakala wa kibinadamu ataweka nia yake kupatana na ile nia ya Mungu, hadi atakapokuwa ameachana na sanamu na kushinda kila mazoea mabaya, kamwe hatafanikiwa katika pambano ila hatimaye atashindwa. Wale ambao watakuwa washindi lazima waingie katika pambano pamoja na wakala wasioonekana, ufisadi ulio ndani ya moyo wapaswa kushindwa, na mawazo yote yapaswa kutiishwa kwa Kristo na kusalimishwa kwa Kristo. Roho Mtakatifu daima yuko kazini akitafuta kutakasa, kusafisha na kuadibisha roho za wanadamu ili kwamba wafae katika jamii ya watakatifu na malaika na kama washindi waweze kuimba wimbo wa ukombozi, wakirudisha utukufu na heshima kwa Mungu na kwa Mwanakondoo katika nyua za mbinguni.. Hatuna adui wa nje ambaye tunaweza kumuogopa. Pambano letu kuu liko katika ubinafsi ambao haujawekwa wakfu, Tutakapoishinda nafsi, tutakuwa zaidi ya washindi kupitia Yeye ambaye alitupenda. Ndugu zangu, kuna uzima wa milele tunaohitaji kuupata. Hebu tupige vita vizuri vya imani. Wakati tulio nao si ujao, lakini sasa.
Lakini msisahau kutenda mema na kushirikiana; maana sadaka kama hizi ndizo zimpendezazo Mungu, (Waebrania 13:16)
Kuishi maisha aliyoishi Mwokozi, kushinda kila shauku yenye ubinafsi, kutimiza wajibu wetu kwa Mungu na kwa wenzetu kwa ujasiri na kwa moyo uliochangamka hutufanya tuwe zaidi ya washindi. Hii hutuandaa kusimama mbele ya kiti kikuu cheupe cha enzi bila mawaa wala makunyazi, tukiwa tumesafisha mavazi yetu ya tabia na kuyasafisha kuwa meupe katika damu ya Mwanakondoo. Nguvu inayotawala watu ya uchu wa chakula itaongoza maelfu kupotea, wakati ambapo kama wangeshinda katika jambo hili, wangekuwa na nguvu ya kimaadili kuwasaidia kupata ushindi juu ya majaribu yote ya shetani. Lakini wale ambao ni watumwa wa uchu wa chakula watashindwa kukamilisha tabia ya Kikristo. Uasi unaoendelea wa mwanadamu kwa miaka elfu sita umeleta matunda ya magonjwa, maumivu na kifo. Tunapokaribia mwisho wa wakati, majaribu ya shetani katika kuendekeza uchu wa chakula yatakuwa yenye nguvu zaidi na magumu kuyashinda.
Ndugu zangu, hebu tuweke yote hayo pembeni, hatuna haki ya kuelekeza mawazo yetu kwetu wenyewe, wala katika vipaumbele vyetu na yote yanayotupendeza. Hatupaswi kutafuta kudumisha kutambulika kwetu kwa namna iliyo ya pekee, wasifu wetu, au ubinafsi wetu, ambao utatutenganisha na watenda kazi wenzetu. Tuna tabia ambayo twapaswa kuidumisha lakini hiyo ni tabia ya Kristo. Tunapokuwa na tabia ya Kristo, tutaweza kuifanya kazi ya Mungu pamoja. Kristo aliye ndani yetu atakutana na Kristo aliye ndani ya wenzetu na Roho Mtakatifu ataleta muunganiko wa mioyo na matendo ambayo yatashuhudia kwa ulimwengu kwamba sisi ni watoto wa Mungu. Hebu Mungu atusaidie kuifia nafsi na kuzaliwa upya, ili Kristo aweze kuishi ndani yetu, kwa kanuni iliyo hai na itendayo kazi, nguvu ambayo itatufanya kudumu kuwa watakatifu.
Maswali ya Kujitathmini:
1. Je ni mapambano gani yaliyo makuu katika maisha yako? Je ni katika mambo gani unahitaji ushindi?
2. Je ni mambo gani yanayokuzuia kutokuwa zaidi ya mshindi? Salimisha mambo hayo kwa Mungu.
Friday, 8 January 2016
Day 4:
Abiding in Christ:
“Abide in Me, and I in you. As the branch cannot bear
fruit of itself, unless it abides in the vine, neither can you, unless you
abide in Me. I am the vine, you are the branches. He who abides in Me, and I in
him, bears much fruit; for without Me you can do nothing.” John 15:4, 5
Those who make a success of
the Christian life will count all things as loss for the excellency of the
knowledge of Christ. Only those who are abiding in Christ can know what true
life is. They realize the value of true religion. They have brought their
talents of influence and means and ability to the altar of consecration,
seeking only to know and do the will of Him who has died to redeem them. (Our
High Calling, p. 8)
It is not a casual touch with
Christ that is needed, but it is to abide with Him. He called you to abide with
Him. He does not propose to you a short-lived blessedness that is realized
occasionally through earnest seeking of the Lord and passes away as you engage
in the common duties of life. Your abiding with Christ makes every necessary
duty light, for He bears the weight of every burden. He has prepared for you to
abide with Him. This means that you are to be conscious of an abiding Christ,
that you are continually with Christ, where your mind is encouraged and
strengthened. (In Heavenly Places, p. 55)
Do not stand outside of
Christ, as many professed Christians of today. To “abide in me, and I in you”
is a possible thing to do, and the invitation would not be given if you could
not do this. Jesus our Saviour is constantly drawing you by His Holy Spirit,
working with your mind that you will abide with Christ. . . . The blessings He
bestows are all connected with your own individual action. Shall Christ be
refused? He says, “Him that cometh to me I will in no wise cast out” (John
6:37). Of another class He says, “Ye will not come to me, that ye might have
life” (John 5:40). (In Heavenly Places, p. 55)
Come unto me, all ye that
labour and are heavy laden, and I will give you rest. (Matt. 11:28, KJV)
Have you, have I, fully
comprehended the gracious call, “Come unto me”? He says, “Abide in me,” not
Abide with Me.
“Do understand My call. Come to Me to stay with Me.” He will freely bestow all
blessings connected with Himself upon all who come to Him for life. He has
something better for you than a short-lived blessedness that you feel when you
seek the Lord in earnest prayer. That is but as a drop in the bucket, to have a
word with Christ. You are privileged with His abiding presence in the place of
a short-lived privilege that is not lasting as you engage in the duties of
life. . . . Will anxiety, perplexity, and cares drive you away from Christ? Are
we less dependent upon God when in the workshop, in the field, in the
market-place? The Lord Jesus will abide with you and you with Him in every
place. (In Heavenly Places, p. 55)
All who receive Christ by
faith become one with Him. The branches are not tied to the vine; they are not
joined to it by any mechanical process of artificial fastening. They are united
to the vine, so as to become part of it. They are nourished by the roots of the
vine. So those who receive Christ by faith become one with Him in principle and
action. They are united to Him, and the life they live is the life of the Son
of God. They derive their life from Him who is life. (In Heavenly Places, p.
56)
Therefore if any man be in
Christ, he is a new creature: old things are passed away; behold, all things
are become new. (2 Cor. 5:17, KJV)
Baptism may be repeated over
and over again, but of itself it has no power to change the human heart. The
heart must be united with Christ’s heart, the will must be submerged in His
will, the mind must become one with His mind, the thoughts must be brought into
captivity to Him. . . . The regenerated man has a vital connection with Christ.
As the branch derives its sustenance from the parent stock and, because of
this, bears much fruit, so the true believer, united with Christ, reveals in
his life the fruits of the Spirit. The branch becomes one with the vine; storm
cannot carry it away; frost cannot destroy its vital properties. Nothing is
able to separate it from the vine. It is a living branch, and it bears the
fruit of the vine. So with the believer. By good words and good actions he reveals
the character of Christ. . . . (In Heavenly Places, p. 56)
Christ has provided means
whereby our whole life may be an unbroken communion with Himself; but the sense
of Christ’s abiding presence can come only through living faith. (In Heavenly
Places, p. 56)
Questions for Personal
Reflection:
1. Is anything (worries,
cares of life, stress, riches) hindering you from abiding in Christ?
2. Where is your
responsibility in making sure that you abide in Christ?
Subscribe to:
Posts (Atom)


