Subscribe:

Friday, 8 August 2014

 Dr Blasious Ruguri:


Maelfu ya washiriki wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato toka Nyanda za juu kusini mwa Tanzania waliojitokeza kumsikiliza Kiongozi wa Kanisa hilo katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati Dr Blasious Ruguri hapa ilikuwa ni Iganzo, Mbeya Agosti 3, mwaka huu, Kiongozi huyo jana aliweka jiwe la msingi katika kanisa la Waadventista Wa Sabato Kirumba na kesho anatarajiwa kuwa mkoani Geita kabla ya kuelekea huko Kigoma katika kuisimika Konferensi mpya ya Magharibi mwa Tanzania

Friday, 1 August 2014

UJENZI WA KANISA LA WAADVENTISTA MBEZI LUIS:


Kiongozi wa Majengo Dr Chacha Matoka akikagua madirisha tayari kwa kazi ya kuyajengea kanisa.
Endelea kutoa Mchango wako ili kazi ya Mungu ikamilike.
 Dr. Blasious Ruguri yuko jijini Mbeya:


Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato,Dr. Blasious Ruguri yuko jijini Mbeya kwa ziara ambapo atashiriki ufunguzi wa Jengo la Makao Makuu ya Konferensi ya Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania iliyoko Iganzo,Shule ya Sekondari ya Mbeya Adventist (MASS) iliyojengwa huko Forest,atatoa Semina kwa Viongozi wa Makanisa ambapo siku ya Sabato ya Agosti 2,mwaka huu washiriki wote wa makanisa ya Waadventista Wa Sabato jijini Mbeya na wajumbe toka makanisa mbalimbali ya Konferensi hii watasali Iganzo ambapo Dr Ruguri atahutubu.

Tuesday, 22 July 2014

Ni George Gachu alipofunga Ndoa siku ya Jumapili ya Tarehe 20/7/2014 katika kanisa la Waadventista Wasabato Mbezi Jijini Dar es salaam.













Monday, 7 July 2014

Ilivyokuwa Tarehe 6/7/2014 katika kanisa la MSINGWA tulipokusanyika Mtaa wa MBEZI LUIS kufanya changizo kwa ajili ya kujenga Nyumba ya Mchungaji wa Mtaa.

                Washiriki wakiwa katika utulivu kanisani

             Kwaya ya Uinjilisti Mbezi Luis wakimtukuza Mungu katika Ibada kuu.



                    Washiriki wakiwa katika usikivu wa pekee katika Ibada

                               Kwa usikivu wa hali ya juu katika Ibada.

  Kwaya ya MSINGWA ikimtukuza Mungu kwa njia ya Nyimbo katika darasa la Watoto.

Sunday, 15 June 2014

MATUKIO YA WABATIZWA KWENYE MKUTANO WA INJILI MBEZI LUIS 13/6/2014 AMBAPO TULIBATIZA WATU 35.

                               Umakini kusikiliza maelekezo kwa Mchungaji.
                  Uhakiki wa majina ukifanyika kwa wabatizwa kabla ya kula kiapo.
          Wabatizwa wakisikiliza kwa umakini maelekezo kutoka kwa Mzee wa kanisa.
                                Wabatizwa wakila kiapo katika Mkutano wa Neno la Mungu
                                       Wakiwa ndani ya Gari tayari kwa kwenda kubatizwa.
  Mchungaji Tirumanywa akitoa maelekezo kwa wabatizwa kabla ya kuanza kuwabatiza.
       Wakiwa wamepanga foleni tayari kwa kuingia kwenye maji na kubatizwa.

Mchungaji Tirumanywa akifanya huduma ya Ubatizo Msasani katika bahari ya Hindi.

                                                Mbatizwa akitoka ndani ya maji.



Wednesday, 4 June 2014

BRAZIL:KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO NCHINI BRAZIL KUTOA HUDUMA ZA KIROHO NA KIJAMII WAKATI WA KOMBE LA DUNIA.

 Makanisa mahalia ya Waadventista Wa Sabato nchini  Brazil yatashiriki  kutoa huduma za kiroho na kijamii kwa maelfu ya mashabiki wa mchezo wa soka wakati wa mashindano ya kombe la dunia  yanayotarajiwa kuanza nchini humo juni 12,mwaka huu.

Shirika la Habari la Kanisa la Waadventista Wa Sabato Duniani (ANN) limeeleza kuwa ,Kanisa la Waadventista Wa Sabato nchini Brazil limepanga kuwatumia vijana na watu wazima wa kanisa hilo katika majiji 12 inakofanyika michuano hiyo kwa kutoa huduma ya maji,matamasha ya uimbaji,maonesho ya masuala ya afya na kujitolea damu.
Mpango huo unaoitwa Tumaini kwa Brazil unalengo la kuwafikia watu toka nchi mbalimbali duniani watakaokuwa  Brazil kushuhudia mashindano hayo  pia utahusisha usambazaji wa vipeperushi na uuzaji wa beji nchini humo ambako shule zitakuwa zimefungwa kwa muda wa siku 32 za michuano hiyo.
Hata hivyo kutakuwa na ugawaji wa vitabu  milioni moja   vya Tumaini Pekee kilichoandikwa na mwinjilisti wa  Alejandro Bullón,magazeti yanayozungumzia matatizo ya biashara ya ngono. 
Areli Barbosa, ambaye ni Mkurugenzi wa Vijana wa Divisheni ya Amerika ya Kusini katika kanisa la Waadventista Wa Sabato amesema mpango huo si kwa ajili ya kuunga mkono michuano ya soka ya Kombe la Dunia bali ni kutoa huduma kwa jamii.