HOTUBA YA ASUBUHI KATIKA MIKUTANO YA WANAMAWASILIANO: 07/06/2016
 
Mr. Atanus Sigoma Mhazini wa ECT akitoa Somo la asubuhi ya leo katika Mikutano ya TAiN inayo endelea hapa Dodoma .
 Pamoja na mengi aliyo yasisitiza yafuatayo ni baadhi:
 1. Huu ni wakati Wakwenda na Technology ili kwenda na kasi kubwa  katika kuinjilisha Dunia. 
 2. Ulimwengu wa sasa  Makarani wa Kanisa wanahitaji Kujua Kompyuta kwa matumizi ya utunzaji wa kumbukumbu za kanisa
 3. Akionesha kuwa kuto endana na technology ni hasara akifafanua hili 
alisema Watu wengi wameshindwa kuendelea na Kazi  au kupata kazi 
kwasababu ya kukosa ujuzi huu.
 4. Akisisitiza swala la kwenda na 
technology alitahadharisha Waumini katika Matumizi sahihi ya technology 
nakwamba Mungu yuko juu ya technology kwani yeye ndiye Technology 
yenyewe.
 5. Akisisitiza matumizi sahihi ya Mitandao alisema nimuhimu
 kujua Kuna mema na Mabaya hivyo tuchunge sana Macho yetu.  Zaburi 
119:37"Unigeuze Macho yangu nisitazame visivyofaa, Unihuishe katika njia
 yako."





 
 
 
0 comments:
Post a Comment